Ofisi ya Waziri Mkuu - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI KUPUNGUZA TATIZO LA WALIMU WA SAYANSI.

Halmashauri ya wilaya ya masasi itafanikiwa kwa kiasi kikubwa kupunguza kufeli kwa masomo ya sayansi katika shule za sekondari baada ya kupata walimu 45 kati ya 74 waliopangwa ni wa masomo ya sayansi huku masomo ya sanaa yakiwa na walimu 27 tu.

Akizungumza wakati wa kuwapokea walimu hao mei 2015 mkurugenzi mtendaji wa halmashauri a wilaya ya masasi bibi Beatrice R Dominic aliishukuru serikali kwa kuwaleta walimu wengi wa masomo ya sayansi, hali itakayosaidia wanafunzi kujifunza masomo ya sayansi kwa ubora.

“walimu wa masomo ya yasansi waliopangwa katika halmashuri ya wilaya ya masasi wamepangiwa vituo yaani shule za kufundisha kutoka serikali kuu ili wasilalamike au kukataa vituo hasa vilivyopo kijijini” alisema Beatrice

Aidha, mpaka tarehe ya mwisho ya kuripoti ni walimu 57 sawa na asilimia 77% wakiwemo wanaume 48 na wanawake 9 tu ndio walioripoti kati yao walimu wa masomo ya sayansi 30 na sanaa 27.